Menu

01. Kutumia mitandao ya kijamii kupata habari

Ama iwe vyanzo vya habari viliyoandikwa kiuandishi wa habari au chombo cha kusambaza habari, mitandao ya kijamii ina jukumu kubwa zaidi katika chumba cha habari cha kidijitali. Ili kufanya kazi katika chumba cha habari cha mtandaoni, ni muhimu kuelewa namna vyombo hivyo vinavyofanya kazi na namna ya kuvitumia kwa ufanisi kadri iwezekanavyo.

Mitandao mikubwa ya kijamii

Ingawa kila kizazi kina mtandao wa kijamii kinaoupendelea zaidi, sasa hivi kuna watu wachache sana ambao hawaitumii. Bila shaka, kuna mtandao mkubwa zaidi wa Facebook, wenye takribani watumiaji hai bilioni tatu kwa mwezi. Hata hivyo, ukubwa wake huo unaanza kupata upinzani kati ya kizazi kipya kutoka mitandao mingine: Instagram, Snapchat na hata TikTok, ni mitandaoni ya kijamii inayoweka mkazo zaidi katika uchapishaji wa picha na video.

Kwa kundi la wanasiasa, michezo na utamaduni, wao wanapendelea zaidi kutumia Twitter, ambayo imejijenga zaidi kama njia kuu ya mawasiliano ya mtandaoni. Bila shaka, hilo la mwisho ndilo muhimu zaidi kwa waandishi wa habari.

Faida yake kwa kazi ya waandishi wa habari

Mitandao ya kijamii inatoa taswira ya kile kinachotokea duniani katika wakati halisi, yote hiyo ikiwa kwenye kompyuta au simu yako. Fuatilia akaunti za mashirika makubwa ya habari duniani na utakuwa na uelewa wa kinachoendelea kwenye kila nyanja ya matukio ndani ya muda mfupi. Fuatilia wabobezi wa eneo mahsusi na utapata habari ya hivi karibuni katika eneo hilo pale jambo lolote linapotokea. Pendelea kuangalia akaunti zenye ushawishi zaidi na zinazozungumzia mambo kwa kina na mara nyingi utashangaa kugundua habari ambayo hukuitarajia. Mitandao ya kijamii ni kama himaya ya habari.

Ukweli kwamba jambo fulani limeandikwa haina maana kwamba ni la kweli.

Kuenea kwa haraka kwa vyanzo vya habari kumesababisha haja ya kuwa makini zaidi. Ingawa mitandao ya kijamii ni vyanzo vyenye nguvu vya usambazaji habari, wakati mwingine inasambaza habari nyingi sana ambazo si kamili na wakati mwingine yenye makosa, pamoja na kudanganya. Mitandao ya kijamii inapaswa kuchukuliwa kama chanzo kingine chochote: akaunti rasmi ya taasisi inaweza kuaminika zaidi kuliko akaunti isiyojulikana mwenyewe, lakini maudhui yake daima yanapaswa kuthibitishwa, kwa kila jambo.